Main menu

Pages

Mwalimu Bloggs

 Tovuti ya kielimu inayosaidia kukuza  Kiswahili miongoni mwa wanafunzi na walimu, kote Afrika Mashariki

LUGHA

Matumizi ya lugha ya Kiswahili yanaangazia sarufi (sheria na kanuni) za lugha hii kwa kuzingatia vipashio vya lugha vinavyotambulika kama vile sauti, aina za maneno, ngeli, nyakati, ukanushaji, uakifishaji, uainishaji wa maneno, aina na muundo wa sentensi na kadhalika.

FASIHI

FASIHI ANDISHI


Fasihi ni moja ya sanaa za lugha. Kwa kuzingatia maana, sifa, na umuhimu wake, katika fasihi tunaangazia vifaa vya Simulizi na Andishi. Miongoni mwa vifaa hivyo, katika ushairi tutazingatia aina za mashairi, muundo wa mashairi na uchambuzi wa mashairi. Hivyo, tutamulika mbinu za lugha na mbinu za sanaa zinazotumika katika fasihi ya Kiswahili.

 

  INSHA

Uandishi wa insha 

Ni utuzi wa mfuatano wa tungo zenye mtiririko unaoelezea kuhusu mada fulani. Pengine unaagizwa shuleni ili kumzoesha mwanafunzi kujieleza kwa maandishi. Jifunze jinsi ya kuandika insha mbalimbali - za kubuni na za kiuamilifu.

 ISIMU JAMII

Ni tawi la isimumbalo huchunguza uhusiano kati ya lugha  na jamiiAidha inajihusisha na athira yeyote ya jamii kama vile desturi za watu, matazamio, na muktadha, katika nyanja za lugha namna inavyotumika. Chini ya taaluma hiyo Tumekuandalia istilahi mbalimbali za Isimu Jamii pamoja na sifa za lugha katika sajili mbalimbali.

 

 

 

Comments

KISWAHILI REVISION PAPERS

KISWAHILI PP1 KCSE PAST PAPERS KISWAHILI MASWALI paper 1 MS KCSE PAST PAPERS KISWAHILI MASWALI paper 2 MS KCSE PAST PAPERS KISWAHILI MA…

Image